Friday 2 April 2010

Fergie: “Rooney kurudi baada ya Wiki 3”
Sir Alex Ferguson, Meneja wa Manchester United, leo amethibitisha kuwa Staa Wayne Rooney atakuwa nje kwa wiki 2 hadi 3 akiuguza enka yake aliyoumia kwenye mechi na Bayern Munich siku ya Jumanne huko Ujerumani.
Ferguson, akiongea leo, amesema: Taifa lipumue sasa! Tumepata nafuu kwani ingekuwa vibaya sana!”
England yote ilikumbwa na wasiwasi kuwa Wayne Rooney ameumia vibaya na huenda akaikosa Fainali za Kombe la Dunia huko Afrika Kusini zinazoanza Juni 11.
Ferguson akaongeza: “Atazikosa mechi zetu muhimu lakini cha muhimu ni kuwa atarudi kabla ya Msimu kwisha na kutusaidia mechi za Ligi zilizobaki.”
Rooney, ambae amefunga mabao 34 Msimu huu, ataikosa mechi ya kesho na Chelsea na ile ya Jumatano ijayo ya marudiano na Bayern Munich.
Mechi nyingine atakayoikosa ni ile ya ugenini ya Ligi Man United watakapocheza na Blackburn lakini ikiwa atapona haraka na vizuri anaweza kuingia dimbani kuivaa Man City hapo Aprili 17

No comments:

Powered By Blogger