Monday 29 March 2010

Eriksson kuongoza Tembo!!
Kocha wa zamani wa England Sven-Goran Eriksson ameteuliwa kuwa Kocha mpya wa Ivory Coast kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia lakini Shirikisho la Soka la Nchi hiyo halikutaja wadhifa huo utakuwa wa muda gani.
Mwezi uliokwisha Ivory Coast walimtimua Kocha wao kutoka Bosnia Vahid Halihodzic kwa kile kilichodaiwa kushindwa kuifikisha Nchi hiyo, maarufu kama ‘Tembo’, Nusu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika lililochezwa Angola mwezi Januari.
Tembo hao, wanaoongozwa na Mchezaji Bora wa Afrika anaechezea Chelsea Didier Drogba, wako Kundi G pamoja na Brazil, Ureno na Korea Kaskazini kwenye Fainali za Kombe la Dunia zitakazoanza huko Afrika Kusini Juni 11.
Eriksson alikuwa Kocha wa England kati ya mwaka 2001 na 2006 na aliiwezesha England kufika Robo Fainali za Kombe la Dunia mara mbili.
Baada ya kuiacha England, Eriksson alikuwa Meneja wa Manchester City na Mexico.
Hivi karibuni alikuwa Mkurugenzi wa Soka wa Klabu ya Notts County.
Kikosi imara chakwaa pipa kwenda Ujerumani
Rio Ferdinand na Wayne Rooney, ambao hawakucheza mechi ya Ligi Kuu ya Jumamosi ambayo Manchester United waliikung’uta Bolton 4-0, ni miongoni mwa Wachezaji 22 waliopanda ndege kwenda Ujerumani ambako Jumanne watacheza mechi ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONS LIGI na Bayern Munich.
Sir Alex Ferguson amethibitisha Wachezaji hao wako fiti na watacheza Jumanne.
Kikosi kamili kilichosafiri ni: Edwin van der Sar, Ben Foster, Tomasz Kuszczak, Gary Neville, Rafael, Nemanja Vidic, Jonny Evans, Rio Ferdinand, Patrice Evra, Ritchie De Laet, Michael Carrick, Darren Fletcher, Darron Gibson, Paul Scholes, Gabriel Obertan, Nani, Antonio Valencia, Ji-sung Park, Ryan Giggs, Wayne Rooney, Dimitar Berbatov, Federico Macheda.

No comments:

Powered By Blogger