Sunday 6 June 2010

PATA MAMBO MAPYA MOTO: http://www.sokainbongo.com/

Benitez kutua Inter?
Bosi wa zamani wa Liverpool Rafael Benitez yupo mbioni kufanya mazungumzo na Inter Milan ili kuziba pengo la Umeneja lililoachwa wazi na Jose Mourinho aliehamia Real Madrid.
Benitez aliacha kazi Liverpool kwa makubaliano na uongozi wa Klabu hiyo Alhamisi iliyopita baada ya kudumu hapo kwa Miaka 6.
Rais wa Inter Milan, Massimo Moratti, ametamka: “Lengo letu ni kuongea nae. Halafu tutajua na kuamua.”
Hata hivyo Benitez atakumbana na mzigo mkubwa huko Inter kwa vile Klabu hiyo chini ya Mourinho ilinyakua Trebo, yaani Vikombe vitatu kwa mpigo pale iliposhinda Serie A, Coppa Italia na UEFA Champions Ligi, na kurudia mafanikio hayo ni kazi ngumu.
Drogba apasuliwa!!
Nahodha wa Ivory Coast, Didier Drogba, amefanyiwa operesheni yenye mafanikio ili kuunga mfupa karibu na kiwiko chake cha mkono wa kulia aliovunjika Ijumaa kwenye mechi ya kirafiki ambayo Ivory Coast iliifunga Japan 2-0.
Drogba aliumia baada ya kuvaana na Sentahafu wa Japan mzaliwa wa Brazil, Marcus Tulio Tanaka.
Lakini hadi sasa haijasemwa kama atapona baada ya muda gani ili aweze kuiwakilisha Nchi yake kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 11 na mechi ya kwanza kwa Ivory Coast ni Juni 15 watakapoivaa Ureno.
Timu nyingine kwenye Kundi la Ivory Coast ni Brazil na Korea Kaskazini.
Rio kubaki na Timu ya England Afrika Kusini
Rio Ferdinand atabaki huko Afrika Kusini na Timu ya England hadi itakapocheza mechi yake ya kwanza ya Kombe la Dunia Jumamosi ijayo dhidi ya USA licha ya kuwa yeye yupo nje ya Mashindano hayo baada ya kuumia goti mazoezini.
Madaktari wamesema atachukua Wiki 4 hadi 6 kupona na hivyo ikabidi aondolewe kwenye Kikosi hicho cha Kombe la Dunia na nafasi yake kujazwa na Beki wa Tottenham Michael Dawson aliesafirishwa haraka toka England na tayari yuko kambini huko Rustenburg, Afrika Kusini.
Nafasi ya Unahodha ya Rio amepewa Naibu wake Steven Gerrard.

No comments:

Powered By Blogger