Sunday 6 June 2010

PATA MAMBO MAPYA MOTO: http://www.sokainbongo.com/



Taifa Stars nje……. Twiga Stars yatinga Fainali!!!
Leo Timu ya Taifa ya Tanzania imebwagwa nje na Rwanda baada ya kupigwa bao 1-0 huko Kigali, Rwanda na hivyo Rwanda itacheza Fainali za CHAN, Mashindano ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani yatakayochezwa huko Sudan Mwakani.
Taarifa kamili za mechi hii tutaleta baadae.
Hapo jana, Timu ya Taifa ya Wanawake, Twiga Stars, imefuzu kuingia Fainali za Kombe la Afrika kwa Wanawake zitakazochezwa huko Afrika Kusini Mwezi Oktoba baada ya kutoka sare na Eritrea kwa bao 3-3 katika mechi iliyochezwa Mjini Asmara, Eritrea na hivyo kufuzu kwa jumla ya goli 11-4.
Twiga Stars walishinda mechi ya kwanza Jijini Dar es Salaam kwa bao 8-1.
Katika mechi ya jana, Twiga Stars, wakiwa chini ya Kocha Charles Boniface Mkwasa, walijikuta wako nyuma kwa bao 3-0 lakini Shujaa alikuwa Asha Rashid aka Mwalala aliepachika bao zote 3 na kuifanya mechi imalizike 3-3.

No comments:

Powered By Blogger