Thursday 10 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Benitez rasmi Inter!!
Meneja wa zamani wa Liverpool Rafael Benitez amethibitishwa rasmi kama Meneja mpya wa Inter Milan baada ya kusaini Mkataba wa Miaka miwili na Mabingwa hao wa Italia na Ulaya.
Klabu ya Inter Milan ilitoa matangazo: “Inter inamkaribisha Rafael Benitez,”
Pia Inter imesema Benitez atatambulishwa rasmi Juni 22 kwenye Mkutano na Wanahabari.
Benitez aliondoka Liverpool wiki iliyopita baada ya kudumu huko kwa Miaka 6.
Pele atoa utabiri Kombe la Dunia 2010….
Mkongwe, aliepachikwa cheo cha Mfalme wa Soka, Pele, kutoka Brazil, kwa mara nyingine tena amejikita kutabiri kwenye Kombe la Dunia ingawa katika Miaka 20 iliyopita utabiri wake umekuwa hautimii na hata kumfanya Straika na Staa wa zamani wa Brazil, Romaria, kutoa kauli: “Pele asiposema kitu ni Mshairi mzuri mno lakini akifungua mdomo hutoa utumbo mtupu!”
Safari hii kwenye Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza kesho Ijumaa Juni 11 huko Afrika Kusini, Pele ameeleza imani yake kuwa ni Spain na Brazil ndio wenye nafasi kubwa kutwaa Kombe la Dunia ingawa ametoa pia matumaini yake kuwa huenda Timu moja ya Afrika ikafika Fainali.
Pele ametamka: “Spain na Brazil ni Timu Bora lakini ni ngumu kusema nani bora zaidi! Ningependa kuiona Brazil ikicheza Fainali na Timu moja toka Afrika! Fainali hizi zitakuwa nzuri kwani maandalizi ni mazuri na zinaendeshwa vizuri!”
Kuhusu Brazil, Pele amesema ni lazima Brazil wajikaze ikiwa watataka kuwa Mabingwa wa Dunia ingawa uwezo wanao.
Pia ameitaja England kuwa ni moja ya Timu ngumu na kumsema Kocha wake Fabio Capello kama ni mzuri huku Kikosi chake kikiwa na Wachezaji wazuri na Wayne Rooney ndio tishio kubwa.
Ballack adai Abramovich ndie aliamua ang’oke Ze Bluzi!!
Michael Ballack amesema uamuzi wa kutokumwongezea Mkataba Chelsea umefanywa na Mmiliki wake Roman Abramovich.
Ballack, Miaka 33, ambae pia amezikosa Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuumia kwenye Fainali ya FA Cup Chelsea ilipoifunga Portsmouth 2-0, ataondoka Chelsea mwisho wa Mwezi huu baada ya Mkataba wake kumalizika.
Ballack amekuwepo Stamford Bridge toka 2006 na amesema: “Siku zote Chelsea ni chaguo langu la kwanza lakini huu si uamuzi wangu ni wa mwenye mali Abramovich.”
Ballack aliongeza kuwa alitambua kitambo kuwa mwisho wake umefika baada ya mazungumzo yake na Chelsea kuhusu kuongeza Mkataba kusimama.
Ballack amesema hayuko tayari kustaafu au kwenda kucheza Marekani au Dubai hivyo atatafuta Klabu yoyote Ulaya na hata kurudi kwao Ujerumani ambako alikuwa Mchezaji wa Bayern Munich kabla kwenda Chelsea.

No comments:

Powered By Blogger