Tuesday 8 June 2010

CHEKI www.sokainbongo.com

Refa adai Rooney ana matusi
Refa aliechezesha pambano la kirafiki hapo jana kati ya England na Platinum Stars, Timu ya huko Rusternburg, Afrika Kusini, Jeff Selogilwe, amedai Wayne Rooney angepewa Kadi Nyekundu kama mechi hiyo ingekuwa ya Kombe la Dunia kwa kumtukana Refa.
Refa huyo alimpa Rooney Kadi ya Njano kwa lugha chafu katika mechi hiyo ambayo England walishinda bao 3-0.
Tangu Rooney apewe Kadi Nyekundu katika Mechi ya Robo Fainali ya Kombe la Dunia Mwaka 2006 England walipocheza na Ureno baada ya kumkanyaga Beki wa Ureno Ricardo Carvalho, Rooney hajawahi kutolewa nje tena.
Lakini Refa Selogilwe amedai: “Ni aibu. Ni Mchezaji mzuri na nampenda lakini tatizo anatukana Marefa. Hilo limenisikitisha.”
Hata hivyo, Refa huyo amesema baada ya Mechi hiyo Rooney alimfuata na kumwomba radhi na kisha kumpa Jezi yake kama zawadi.
Nani nje Kombe la Dunia
Ureno imepata pigo baada ya Winga wa Manchester United, Nani, kujitoa kushiriki Fainali za Kombe la Dunia kufuatia kuumia bega.
Habari hizo za kuumia kwa Nani zimethibitishwa na Kocha wa Ureno Carlos Queiroz ambae tayari ameshamwita Mchezaji wa Benfica, Ruben Amorim, kuchukua nafasi ya Nani.
Nani aliumia bega mazoezini wiki iliyopita na awali ilidhaniwa si maumivu makubwa lakini uchunguzi wa kina umedhihirisha hawezi kupona mapema na kucheza Kombe la Dunia ambalo Ureno wanacheza Mechi yao ya kwanza Juni 15 na Ivory Coast.
Man City kuwaondoa wachezaji watatu.
Wachezaji watatu wa Manchester City, Martin Petrov, Sylvinho na Benjani wataondolewa Klabu hiyo kabla Msimu ujao kuanza hapo Agost 14.
Petrov, mwenye Miaka 31 na ni Raia wa Bulgaria, alisainiwa Mwaka 2007 wakati huo Timu ikiwa chini ya Meneja Sven-Goran Eriksson lakini amemudu kucheza Mechi 57 tu na kufunga bao 15 kwa vile amekuwa akiumia mara kwa mara.
Nae Beki toka Brazil, Sylvinho, Miaka 35, alisaini Mkataba wa Mwaka mmoja Agosti mwaka jana lakini amemudu kuanza Mechi 9 tu tangu wakati huo.
Mchezaji mwingine atakaeondolewa ni kutoka Zimbabwe, Benjani, Miaka 31, alietua Man City Mwaka 2008 lakini ameshindwa kupata namba na nusu ya pili ya Msimu wa Ligi Kuu wa 2009/10 alipelekwa Sunderland kwa mkopo.

No comments:

Powered By Blogger