Sunday 6 June 2010

PATA MAMBO MAPYA MOTO: http://www.sokainbongo.com/

Nigeria 3 Korea Kaskazini 1
• Washabiki wavamia milango, wengi waumia!
Washabiki 13 pamoja na Polisi mmoja walikimbizwa Hospitali baada ya kuvamia milango ya Uwanja wa Makhulong huko Johannesburg, Afrika Kusini, wengi wao wakiwa Mashabiki wa Nigeria, ili kuona pambano la kirafiki kati ya Korea Kaskazini na Nigeria lililofanyika leo Jumapili Juni 6.
Ingawa hakuna aliefariki, Watu kadhaa walijeruhiwa katika harakati za kutaka kuingia Uwanjani katika mechi hiyo ambayo ilikuwa haina kiingilio ila zilitolewa Tiketi za mwaliko za bure wa kuingia Uwanja wa Makhulong unaoweza kuchukua Watu 10,000 tu.
Uwanja huo wa Makhulong si mmoja wa Viwanja vitakavyotumika kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia.
Hata hivyo mechi hiyo ya kirafiki iliendelea na Nigeria waliifunga Korea Kaskazini bao 3-1.
Mabao yalifungwa na Yakubu Aiyegbeni, dakika ya 17, Victor Obinna, dakika ya 62 kwa penalti na Obafemi Martins kwa upande wa Nigeria.
Bao la Korea Kaskazini lilifungwa na Jong Tea-Se dakika ya 61.

No comments:

Powered By Blogger