Friday 11 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Bafana, El Tri ngoma ngumu!
Afrika Kusini 1 Mexico 1
Mechi ya ufunguzi ya Fainali za Kombe la Dunia kati ya Wenyeji Afrika Kusini na Mexico iliyochezwa Soka City, Soweto ilimalizika kwa sare ya 1-1.
Matokeo haya hayakuwafurahisha Afrika Kusini lakini ukweli ni kwamba ni matokeo bora kwao kwa vile Mexico walitawala muda mwingi na hasa Kipindi cha Kwanza walikosa mabao ya wazi kadhaa.
Hadi mapumziko mabao yalikuwa 0-0.
Kipindi cha Pili, dakika ya 55, Siphiwe Tshabalala aliachia mzinga uliokwenda juu na kutikisa nyavu na kufanya Soweto yote itetemeke kwa Vuvuzela na shangwe zilizotoka ndani ya Uwanja wa Soka City.
Mexico walisawazisha kwenye dakika ya 79 baada ya pasi ndefu kumkuta Beki Rafael Marquez, aliepanda, akiwa peke yake na kumchambua Kipa Khune.
Hata hivyo, Bafana Bafana wangeweza kushinda mechi hii kama Mphela angetuliza akili pale alipopewa bonge la pande na kujikuta yuko yeye na Kipa Perez lakini kutaka kufunga kifundi kulisababisha mpira huo ugonge mwamba na kutoka.
Mechi inayofuata kwa Bafana ni Juni 16 watakapocheza na Uruguay Uwanja wa Loftus Versfed, Pretoria.
Mexico watacheza Juni 17 na Ufaransa huko Uwanja wa Peter Mokaba, Polokwane.
Timu:
South Africa: Khune, Gaxa, Mokoena, Khumalo, Thwala,
Tshabalala, Dikgacoi, Letsholonyane, Modise, Pienaar, Mphela.
Akiba: Josephs, Masilela, Ngcongca, Sibaya, Davids, Booth, Parker, Nomvethe, Moriri, Sangweni, Walters, Khuboni.
Mexico: Perez, Aguilar, Rodriguez, Osorio, Salcido, Torrado, Marquez, Juarez, Giovani, Franco, Vela.
Akiba: Ochoa, Barrera, Castro, Blanco, Hernandez, Moreno, Guardado, Magallon, Torres, Bautista, Medina, Michel.
Refa: Ravshan Irmatov (Uzbekistan

No comments:

Powered By Blogger