Saturday 12 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Nigeria yalala!
Leo, Argentina imewafunga Nigeria bao 1-0 katika mechi ya pili ya pili Kundi B iliyochezwa Uwanja wa Ellis Park huko Johannesburg.
Awali leo katika mechi nyingine ya Kundi B, Korea Kusini iliwapiga Ugiriki bao 2-0.
Ni bao la Mkongwe na Mchezaji wa zamani wa Manchester United, Beki Gabriel Heinz, alilofunga kwa kichwa baada ya kona ya Mkongwe mwingine ambae pia aliwahi kuichezea Manchester United, Juan Sebastian Veron, la dakika ya 6 ndilo lililowaua Nigeria.
Ingawa Argentina walionekana ni hatari sana, lakini Nigeria walipata nafasi nyingi za wazi za kusawazisha lakini wakazipoteza.
Kwa upande wa Nigeria Shujaa mkubwa ni Kipa wao Enyeama alieokoa bao nyingi za wazi na hasa kumzuia Lionel Messi kupata bao wakati alipata nafasi nyingi.
Mechi zinazofuata kwa Timu hizi ni Juni 17 Nigeria v Ugiriki na Argentina v Korea Kusini.
Timu:
Argentina: Romero; Gutierrez, Demichelis, Samuel, Heinze; Mascherano, Veron, Di Maria; Messi, Higuain, Tevez.
Nigeria: Enyeama; Odiah, Shittu, Yobo, Taiwo; Etuhu, Haruna, Kaita; Ogbuke Obasi, Yakubu, Obinna.
Refa Wolfgang Stark (Germany)

No comments:

Powered By Blogger