Friday 11 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

PATI ya KOMBE LA DUNIA J’BURG!!!
Maelfu ya Watu walifurika na kuselebuka Uwanja wa Orlando, Soweto Jijini Johannesburg, Afrika Kusini huku wakiimba kwa furaha kusheherekea kuanza kwa Fainali za Kombe la Dunia ambazo kwa mara ya kwanza kabisa zitachezwa Barani Afrika kuanzia leo hadi Julai 11.
Watu waliimba, kupiga makofi, kucheza na kufurahia huku kibaridi kikali kikizizima.
Konseti hiyo ilipeperushwa Duniani kote huku Mastaa kina Alicia Keys, Angelique Kidjo na Vusi Mahlasela wakinguruma stejini.
Shakira ndie aliehitimisha sherehe hizo kwa Wimbo ‘Waka Waka This Time for Afrika’ alioimba na Kikundi cha Soweto Freshly Ground.
Watoto kwa Wakongwe wa Afrika Kusini walijumuika kuimba ‘Shosholoza’, Wimbo maarufu wa huko Afrika Kusini.
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, na Rais wa FIFA, Sepp Blatter, walikuwa miongoni mwa kadamnasi hiyo.
Makusanyo toka mapato ya Konseti hiyo yatatumiwa kujenga Vituo 20 vya Afya, Elimu na Kufundisha Soka sehemu mbalimbali Afrika.
Askofu Desmond Tutu alipopanda jukwaani umati ulilipuka kwa kelele za : “Tutu, Tutu!”
Askofu Tutu akawaambia: “Ni kama niko ndotoni- niamsheni!”

No comments:

Powered By Blogger