Wednesday 9 June 2010

CHEKI www.sokainbongo.com

Robinho ng’o kurudi Man City!!
Mawakala wa Robinho wanategemewa kuruka hadi Manchester wiki ijayo ili kwenda kuwajulisha Manchester City kuwa Mteja wao hana nia
ya kurudi huko baada ya Mkataba wake wa mkopo kuchezea Santos ya Brazil kumalizika.
Robinho, aliesajiliwa kwa dau la rekodi huko Uingereza la Pauni Milioni 32.5 Septemba 2005 kutoka Real Madrid, alikuwa hapendezewi na maisha ya Manchester na pia kutoridhika na Meneja wa Man City, Roberto Mancini, ambae Robinho amemwelezea kama Mtu anaekosa uwezo wa kuongoza Timu.
Msimamo wa Man City ni kuwa wanamtaka Robinho arudi Klabuni hapo Agosti 3 tayari kwa Msimu mpya wa Ligi Kuu lakini kuna kila dalili Man City wanajua Robinho harudi tena hapo.
Kuna mipango ya chinichimi ya kumpeleka Robinho FC Barcelona ingawa Mawakala wake hawajathibitisha hilo mbali ya kugusa tu kijuujuu kuwa Mchezaji yeyote Yule atafurahi kuchezea Barca.
Ballack, Cole na Belletti kwa heri Ze Bluzi!!
Chelsea imethibitisha Wachezaji wake watatu, Joe Cole, Michael Ballack na Juliano Belletti, wataondoka Klabu hiyo baada ya Mikataba yao kumalizika mwishoni mwa Mwezi huu.
Wakati Belletti, mwenye umri wa miaka 33, hakupewa ofa yeyote ya kuongezewa Mkataba, Cole na Ballack walipewa ofa mpya ya nyongeza ya Mikataba yao lakini hawakuridhika nayo na hivyo mazungumzo yakavunjika.
Belletti, Raia wa Brazil, alijiunga na Chelsea Mwaka 2007 akitokea Barcelona na amechezea Chelsea mechi 54 na kufunga bao 5.
Cole, Miaka 28, alijiunga na Chelsea Mwaka 2003 akitokea West Ham na hivi sasa yuko huko Afrika Kusini na Kikosi cha England kinachosubiri kucheza Fainali za Kombe la Dunia.
Ballack, Miaka 33, alijiunga na Chelsea Mwaka 2006 na alitegemewa kuiongoza Nchi yake Ujerumani kama Nahodha huko Afrika Kusini kwenye Kombe la Dunia lakini akaumizwa kwenye Fainali ya FA Cup Chelsea ilipocheza na Portsmouth na kushinda 2-0 hapo Mei 15 na hivyo kuikosa michuano hiyo ya Dunia.
Fulham wamsaini Senderos
Fulham imekamilisha taratibu za kumsaini Difenda wa Arsenal Philippe Senderos kwa Mkataba wa Miaka mitatu.
Senderos amejiunga na Fulham kama Mchezaji huru baada ya Mkataba wake huko Arsenal kumalizika.
Mchezaji huyo ambae yuko Afrika Kusini na Uswisi kwenye Kombe la Dunia aliichezea Everton kwa mkopo nusu ya mwisho ya Msimu wa Ligi Kuu wa 2009/10 uliomalizika Mei 9 na Msimu wa nyuma yake alikaa Mwaka mzima huko AC Milan akicheza kwa mkopo.
Sendoros, Miaka 25, alijiunga na Arsenal Mwaka 2003 akitokea Servette ya Uswisi lakini amekuwa hana namba ya kudumu.

No comments:

Powered By Blogger