Saturday 12 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com
Kanu amshambulia Maradona, Kocha asema hawamjali Messi!!
Nahodha wa Nigeria, Nwankwo Kanu, amemshambulia Kocha wa Argentina, Diego Maradona, kwa kauli yake kuwa Super Eagles watatumia mabavu na kuwaumiza Argentina ili kuwadhibiti.
Maradona pia alidai Nigeria itawaandama Wachezaji wake Mastaa kama Lionel Messi ili kuwachezea vibaya na kuwaumiza.
Leo Jumamosi Juni 12, saa 11 jioni saa za bongo, Argentina na Nigeria zinakumbana kwenye mechi ya Kundi B Uwanja wa Ellis Park, Johannesburg.
Kanu, akionyesha kukasirishwa na kauli za Maradona, ametamka: “Tuko hapa kucheza Soka. Haitakuwa tofauti na mechi nyingine. Sisi ni wapiganaji lakini tunacheza Soka.”
Nae Kocha wa Nigeria, Lars Lagerbach, amesema Timu yake haina plani yeyote ya kumdhibiti au kumchezea vibaya Lionel Messi.
Lagerbach amesema: “Sisi tunacheza na Argentina na sio Messi. Hakuna Mchezaji wetu atakaepewa kazi maalum ya kumchunga Messi.”
Kocha huyo akaongeza kwa kusema kuwa ukicheza na Timu nzuri kama Argentina ambao ina Wachezaji wengi wenye vipaji ni muhimu kucheza vizuri Kitimu.
Lagerback amesema: “Tukiwa na mpira, tutashambulia kwa akili. Tukiwa hatuna mpira, tutajihami. Na kama Wapinzani wetu ni bora kupita sisi, itabidi tujihami sana kuliko kushambulia!”

No comments:

Powered By Blogger