Ugiriki 0 Korea Kusini 2

Hadi mapumziko Korea walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Kipindi cha Pili, Nahodha wa Korea Kusini, ambae pia ni Mchezaji wa Manchester United, Park Ji-Sung aliinasa pasi mbovu ya Vyntra katikati ya upande wa Ugiriki na kuchanja mbuga huku akiwatambuka Mabeki kadhaa wa Ugiriki na kumchambua Kipa Tzorvas na kupiatia Korea bao la pili, hiyo ikiwa dakika ya 52.
Korea ingeweza kupata bao zaidi ya mbili kama wangetuliza bongo kwani waliizidi kila kitu Ugiriki.
Mechi zinazofuata kwa Timu hizi ni Juni 17 Korea Kusini v Argentina na Ugiriki v Nigeria.
Timu:
Greece: Tzorvas, Torosidis, Papadopoulos, Vyntra, Seitaridis, Samaras, Tziolis, Katsouranis, Karagounis, Charisteas, Gekas.
Akiba: Chalkias, Patsatzoglou, Spyropoulos, Moras, Salpingidis, Kyrgiakos, Ninis, Papastathopoulos, Kapetanos, Malezas, Prittas, Sifakis.
South Korea: Jung, Cha, Cho, Jung-Soo Lee, Young-Pyo Lee, Chung-Yong Lee, Ki, Jung-Woo Kim, Ji-Sung Park, Chu-Young Park, Yeom.
Akiba: Woon-Jae Lee, Oh, Hyung-il Kim, Nam-Il Kim, Bo-Kyung Kim, Ahn, Seung-Youl Lee, Jae-Sung Kim, Dong-Jin Kim, Dong-Gook Lee, Kang, Young-Kwang Kim.
Refa: Michael Hester (New Zealand)
No comments:
Post a Comment