Saturday 12 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Ugiriki 0 Korea Kusini 2
Korea Kusini leo imeanza vyema kampeni yao kwenye Fainali za Kombe la Dunia walipoidunda Ugirki kwa bao 2-0 katika mechi ya Kundi B iliyochezwa Uwanja wa Nelson Mandela huko Port Elizabeth.
Korea Kusini walifunga bao la kwanza kwenye dakika ya 7 baada ya frikiki ya Ki karibu na kibendera cha kona kuingizwa ndani ya boksi na kumfanya Katsouranis kumchanganya Kipa Tzorvas na mpira kumkuta Lee Jung-soo alieupachika wavuni.
Hadi mapumziko Korea walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Kipindi cha Pili, Nahodha wa Korea Kusini, ambae pia ni Mchezaji wa Manchester United, Park Ji-Sung aliinasa pasi mbovu ya Vyntra katikati ya upande wa Ugiriki na kuchanja mbuga huku akiwatambuka Mabeki kadhaa wa Ugiriki na kumchambua Kipa Tzorvas na kupiatia Korea bao la pili, hiyo ikiwa dakika ya 52.
Korea ingeweza kupata bao zaidi ya mbili kama wangetuliza bongo kwani waliizidi kila kitu Ugiriki.
Mechi zinazofuata kwa Timu hizi ni Juni 17 Korea Kusini v Argentina na Ugiriki v Nigeria.
Timu:
Greece: Tzorvas, Torosidis, Papadopoulos, Vyntra, Seitaridis, Samaras, Tziolis, Katsouranis, Karagounis, Charisteas, Gekas.
Akiba: Chalkias, Patsatzoglou, Spyropoulos, Moras, Salpingidis, Kyrgiakos, Ninis, Papastathopoulos, Kapetanos, Malezas, Prittas, Sifakis.
South Korea: Jung, Cha, Cho, Jung-Soo Lee, Young-Pyo Lee, Chung-Yong Lee, Ki, Jung-Woo Kim, Ji-Sung Park, Chu-Young Park, Yeom.
Akiba: Woon-Jae Lee, Oh, Hyung-il Kim, Nam-Il Kim, Bo-Kyung Kim, Ahn, Seung-Youl Lee, Jae-Sung Kim, Dong-Jin Kim, Dong-Gook Lee, Kang, Young-Kwang Kim.
Refa: Michael Hester (New Zealand)

No comments:

Powered By Blogger