Thursday 10 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com


Ni Bondeni Taimu....KOMBE LA DUNIA 2010!!!
Hii ni mara ya kwanza kwa Afrika kuwa Wenyeji wa Fainali za Kombe la Dunia na Afrika Kusini ndio Wenyeji wa kihistoria wa Mashindano haya makubwa kabisa Duniani na ambayo ni Fainali za 19 za Kombe la Dunia.
Ijumaa Juni 11, Soccer City, Uwanja uliopo Kitongoji cha Soweto, Johannesburg unaoingiza Watu 94,000, ndio utakaofanyiwa sherehe za ufunguzi na pia Mechi ya ufunguzi kufanyika kati ya Wenyeji Bafana Bafana na El Tri, yaani Mexico.
Inaaminika Madiba, Mzee Nelson Mandela, Miaka 91, atakuwepo japo kwa muda mdogo tu wakati wa ufunguzi huo.
Mechi hii itaanza saa 11 jioni saa za bongo.
Sherehe hizo za ufunguzi zinategemewa kudumu kwa dakika 40 na zitaanza saa 9 mchana, bongo taimu, huku Mmarekani R&B Staa R Kelly, akiwa mmoja wa Watumbuizaji 1581 wakiwemo Wacheza densi, Waimbaji na wengineo.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, ambae atakuwepo Uwanjani hapo, ametamka: “Afrika Kusini imefufuka na haitabaki nyuma baada ya Kombe la Dunia!”
Aliongeza: “Nelson Mandela amefanya kazi kubwa ya kutuwezesha sisi kuwa Wenyeji wa Mashindano haya. Tunamtunukia Kombe la Dunia yeye! “
Alhamisi, Juni 10, kuna konseti huko Soweto ikitumbuizwa na kina Shakira na wimbo spesheli kwa Kombe la Dunia ‘Waka Waka Time for Africa’, Black Eyed Peas, Alicia Keys, Hugh Masekela, Kidjo na wengineo.
Mashindano haya yanajumuisha Nchi 32 na Mwandaaji Mkuu toka Afrika Kusini, Danny Jordaan, amezungumza: “Watu walisema hakuna Nchi ya Afrika inaweza hili! Huu ni wakati bora katika Miaka 80 ya historia ya Kombe hili! Hii ni ndoto iliyotimia kwangu! Wale waliokuwa hawaamini sasa wamekuwa ndio waaminifu wakubwa!”
Mechi za Fainali za Kombe la Dunia zitachezwa katika Miji ya Johannesburg, yenye Viwanja viwili, Soccer City na Ellis Park, na Miji mingine ni Cape Town, Pretoria, Polokwane, Rustenburg, Bloemfontein, Port Elizabeth, Durban na Nelspruit.
Fainali ya Kombe la Dunia ni Julai 11.

No comments:

Powered By Blogger