Tuesday 8 June 2010

CHEKI www.sokainbongo.com

Padri aadhibiwa kwa uhuni kwenye Soka
Thessaloniki, Ugiriki
Padri wa Kigiriki ambae ni Shabiki lililokubuhu la Soka ameadhibiwa na Kanisa la Orthodox huko Mji wa Thessaloniki, Ugiriki kwa kufanya uhuni wakati akishabikia Klabu anayoisapoti.
Padri Christos ni Shabiki wa kutupwa wa Klabu kubwa na maarufu ya PAOK FC inayosifika kwa kuwa na Mashabiki wenye fujo huko Ugiriki na kawaida Padri huyo huenda kutazama Mechi zake akiwa na Majoho ya Upadre huku amejitanda skafu ya PAOK FC.
Mashabiki wenzake wa PAOK wamembatiza jina la ‘Papa PAOK’.
Padre Christos, mwenye umri wa miaka 60 na kitu, alijijengea sifa mbaya pale aliponaswa kwenye mikanda ya Video iliyozagaa mtandaoni kwenye tovuti ya You Tube ikimwonyesha yuko katikati ya Mashabiki waliokuwa wakiwatukana Wapinzani wao na nyingine zilionyesha genge la PAOK FC wakiimba: “Padre ndie Mungu.”
Kanisa lake likachoshwa na vitimbwi vya Papa PAOK na wakaamua kumwadhibu kwa kumshusha wadhifa wake na pia kumpiga marufuku kushiriki Magenge ya Washabiki.
Hatua ya Kanisa hilo imewaudhi Washabiki wa PAOK ambao wameanzisha Kampeni kwenye mtandao wa Facebook inayoitwa “Mfungulieni Papa PAOK”.
Rio: ‘Heskey hana kosa!’
Rio Ferdinand amesisitiza Emile Heskey sio wa kulaumiwa kwa kuumia kwake kulikomfanya alikose Kombe la Dunia.
Beki huyo wa Manchester United na Nahodha wa England aliumia goti Ijumaa iliyopita mazoezini alipovaana na Heskey walipokuwa wanagombea mpira na maumivu hayp yamemfanya awe nje ya uwanja kwa wiki 6 hivyo kuzikosa Fainali za Kombe la Dunia zinazoanza Juni 11.
Ingawa hawezi kucheza, Ferdinand ameamua kubaki na Kikosi cha England huko Rusternburg, Afrika Kusini hadi baada ya Mechi ya Kwanza ya England Jumamosi ijayo Juni 12 England itakapocheza na USA.
Rio ametamka: “Ni bahati mbaya! Ni eksidenti tu!”
Rio aliongeza kuwa alitambua palepale alipoumia kuwa ndoto yake ya kuiongoza England kama Nahodha imekwisha.
Rio amesema: “Inavunja moyo lakini nimeshakubali ukweli. Usiku wa kwanza ulikuwa mgumu kila kitu nilikifikiria sana. Kuiongoza Nchi yako katika Mashindano makubwa ni ndoto kubwa. Inasikitisha!”
Kombe la Dunia: Utabiri wa Pele
Straika wa zamani wa Brazil na Mtu anaesifiwa kuwa ndie Mchezaji Bora wa Soka katika Historia aliepewa cheo cha ‘Mfalme wa Soka’ ni Pele lakini siku zote utabiri wake kwenye Soka umekuwa si sahihi na haupewi uzito mkubwa na Wadau.
Hali hiyo imemfanya hata Staa wa zamani wa Brazil, Straika ambae alipata sifa kubwa, Romario, kutamka: “Pele akikaa kimya ni Mshairi mzuri lakini akifungua mdomo tu hubwabwaja utumbo tu!”
Ufuatao ni utabiri wa Pele kuhusu Kombe la Dunia katika Miaka 20 iliyopita:
1990
UTABIRI: "Italy ndio washindi"
MATOKEO: Italy walifungwa na Argentina kwenye Nusu Fainali na Ujerumani Magharibi wakawa Mabingwa wa Dunia.
1994
UTABIRI: "Kwangu mimi Colombia ndio Timu Bora. Haimaanishi watashinda Kombe la Dunia lakini watakuwa moja ya Timu 4 kwenye Nusu Fainali. Brazil wana Wachezaji wazuri lakini Kitimu si wazuri. Ujerumani ni wazuri Kitimu.”
MATOKEO: Colombia wanatolewa mapema na Beki alejifunga mwenyewe Andres Escobar anapigwa risasi na kuuliwa waliporudi kwao huko Colombia.
Ujerumani wanatolewa Robo Fainali.
Brazil wanachukua Ubingwa wa Dunia.
1998
UTABIRI: "Spain ndio Washindi na siku zote naamini Brazil watafika Fainali. Ufaransa ina Wachezaji wazuri wanaocheza Kitimu na wako nyumbani. Wana nafasi nzuri kufika Fainali. England wana Meneja mzuri, staili nzuri na Timu ngumu.”
MATOKEO: Spain wanatolewa kwenye Makundi na Ufaransa inaifunga Brazil kwenye Fainali.
2002
UTABIRI: "Brazil wamekuwa hawachezi vizuri, hawachezi Kitimu. Kuna msululu wa Timu Bora hivi sasa zikiwemo Argentina, Ufaransa, Italia na Ureno lakini hamna moja bora kupita wenzake. Chini yao zipo Ujerumani, England na Spain.”
MATOKEO: Argentina, Ufaransa na Ureno zinabwagwa kwenye Makundi.
Italia wanatolewa Raundi ya Pili na Korea Kusini.
Brazil wanachukua Ubingwa wa Dunia.
2006
UTABIRI: "Timu 4 za Nusu Fainali ni Brazil, Argentina, England na France"
MATOKEO: England, Argentina na Brazil zote zinatolewa Robo Fainali.
Italy anamfunga Ufaransa Fainali na kuwa Bingwa.
UTABIRI WA PELE MKUBWA: “Nchi ya Afrika itashinda Kombe la Dunia kabla Mwaka 2000.”
MATOKEO: Hadi leo hamna hata Nchi moja ya Afrika iliyovuka Robo Fainali ya Kombe la Dunia

No comments:

Powered By Blogger