Monday 7 June 2010

PATA MAMBO MOTO: www.sokainbongo.com

BONGO LEO NI SAMBA PATI!!!!
Leo Jiji la Dar es Salaam litawaka moto baada ya Magwiji wa Soka Duniani Brazil kutua Bongo wakitokea Afrika Kusini hapo jana usiku na leo kuanzia saa 12 jioni saa za Bongo watashuka Uwanja wa Taifa kuchuana na Tanzania kwenye mechi ya kirafiki.
Brazil, ambao wako kambini Afrika Kusini, wakisubiri kuanza kwa Fainali za Kombe la Dunia, walicheza Harare, Zimbabwe Jumatano iliyopita na wakaifunga Zimbabwe bao 3-0 kwa bao za Bastos, Robinho na Elano.
Pichani ni Staa Kaka akiwa na Meneja wake Dunga ambae ndie alikuwa Nahodha wa Brazil waliochukua Ubingwa wa Dunia huko USA Mwaka 1994.
Timu ya Taifa ya Tanzania jana ilikuwa Kigali, Rwanda na ilifungwa na Nchi hiyo bao 1-0 na kutupwa nje ya Fainali za CHAN, Mashindano ya Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani.
Timu hiyo ilitegemewa kurudi Dar es Salaam leo asubuhi.
Mechi hii ya leo ya Tanzania v Brazil itarushwa moja kwa moja kwenye TV na kushuhudiwa kwenye zaidi ya Nchi 160 Duniani [ikiwemo Qatar alipo Mdau wa Blogu hii na itaonyeshwa na Al Jazeera Sports +1].
Kwa bahati mbaya, Wabongo watakaoshindwa kwenda huko Uwanja wa Taifa hawataiona mechi hii moja kwa moja kupitia TV kwa madai kuwa haki ya kurushwa kwa matangazo wanayo Globo TV ya Brazil na hakuna Kituo chochote cha Tanzania kilichopewa haki ya kurusha laivu ila wataruhusiwa kuionyesha mechi hiyo baadae kwa kuirekodi.

No comments:

Powered By Blogger