Monday 7 June 2010

Cheki www.sokainbongo.com

SAMBA PATI Bongo:
Taifa Stars 1 Brazil 5
Brazil wameifunga Tanzana mabao 5-1 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete pamoja na maelfu ya Watu wengine.
Brazil, ambao wako Afrika Kusini kwa ajili ya Kombe la Dunia, walipanga Kikosi chao chote kamili wakiwemo Masupastaa Kaka, Robinho, Fabiano, Maikon, Lucio na wengine ambao Bongo wamezoeleka kuonekana kwenye luninga tu.
Ingawa Tanzania walifungwa lakini mabao hayo, hasa ya kipindi cha kwanza, yametokana na uzembe wa Mabeki na si kwa sababu ya ufundi mkubwa wa Brazil ingawa walionyesha ni wepesi mno kutumia makosa ya Mabeki.
Kipindi cha kwanza Tanzania walijitahidi mno kushambulia na mara kadhaa walimpa misukosuko Kipa wa Brazil anaedakia Tottenham, Gomez, alielazimika kuokoa mipira kadhaa hasa toka kwa Mrisho Ngassa ambae hakika kiwango chake ni cha juu.
Mabao mawili ya kwanza ya Brazil yalifungwa na Robinho dakika ya 13 na 33.
Hadi mapumziko Tanzania 0 Brazil 2.
Kipindi cha pili, Brazil walionyesha kuongeza kasi, kutulia na kutumia utaalam wa juu kidogo na kwenye dakika ya 53, Ramirez alieingizwa kipindi hicho kuchukua nafasi ya Mkongwe Gilberto aliachia fataki iliyomshinda Kipa Mohamed.
Dakika ya 75 krosi ya Fulbeki Maikon aliepanda ilikoswa na Kipa Mohamed na Kaka akamalizia na kuipatia Brazil bao la 4.
Lakini Tanzania ikafanya kitu ambacho Nchi nyingi zimeshindwa kukifanya tangu Oktoba Mwaka jana pale walipoitoboa ngome ya Brazil kwa mara ya kwanza kupitia Jabir Aziz alieingia Kipindi cha Pili alipofunga bao kwa kichwa kwenye dakika ya 86.
Brazil wakafunga kitabu cha mabao dakika za majeruhi kwa Ramirez kupachika bao lake la pili na la 5 kwa Brazil.
Vikosi vilikuwa:
Tanzania: Mohamed, Yondani, Cannavaro, Kigi, Mgosi, Ngassa, Shadrak, Nizar Khalfan, Makasi [Aziz], Mwasiga, Nyoni [Nurdin Bakari]
Brazil: Gomez, Maikon, Lucio [Luisao], Juan, Bastos [Gilberto], Elano [Dani Alves], Gilberto [Ramirez], Felipe Melo [Josue], Robinho, Kaka, Fabiano Nilmar]

No comments:

Powered By Blogger