Saturday 12 June 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com


KOMBE LA DUNIA: Mechi Jumamosi Juni 12
England v USA
KIWANJA: Royal Bafokeng, Rustenburg
TAREHE: 12 JUNI 2010
SAA: 3 na nusu usiku [Bongo]
HABARI ZA TIMU:
Timu ya England inabeba matumaini makubwa ya Nchi yao ambayo wengi wanategemea makubwa toka kwao na zigo hilo kubwa na zito liko mabegani mwa Straika Wayne Rooney.
England, chini ya Meneja kutoka Italia, Fabio Capello, itawavaa ‘wapwa zao’ USA.
Capello hajakitaja Kikosi chake cha Kwanza na kitakachocheza na USA lakini mwenyewe ameshasema anajua nani watacheza.
Ingawa Wadau wanaweza kuotea Timu itakuwa ipi lakini nafasi ya Kipa ndio haina uhakika kabisa na yeyote kati ya Makipa watatu, David James, Rob Green na Joe Hart, anaweza kupangwa.
Katika Difensi, Capello itabidi amtafute nani atakuwa patna wa John Terry baada ya Nahodha wao, Rio Ferdinand, kuumia na kutolewa kwenye Fainali hizi.
Hivyo, Capello itabidi amchague mmoja kati ya Ledley King, Matthew Upson, Jamie Carragher au Michael Dawson awe patna wa John Terry.
Kwenye Kiungo, bado Gareth Barry hayuko fiti hivyo huenda Michael Carrick, Steven Gerrard na Frank Lampard wakacheza kwa pamoja.
Mbele, Rooney tayari namba yake ipo na swali lililobaki ni nani atakuwa patna wake kwenye mashambulizi. Patna huyo atatoka kati ya Peter Crouch, Emile Heskey au Jermain Defoe.
USA, iliyo chini ya Kocha Bob Bradley, si Timu mchekechea ni Timu ngumu mno na yenye Wachezaji wapiganaji wazuri.
USA, Mwaka jana, waliitoa Spain na kutinga Fainali ya Kombe la Mabara na kufungwa na Brazil kwa bao 1-0.
USA ina Wachezaji kadhaa wanaocheza Ligi Kuu Engand nao ni Kipa Tim Howard wa Everton, Jonathan Spector alieanzia kucheza Manchester United na sasa yupo West Ham, Landon Donovan, Mchezaji wa Timu ya David Beckham LA Galaxy ya Marekani ambae alichezea Everton kwa mkopo, Clint Dempsey wa Fulham na Jozy Altidore wa Hull City.
Argentina v Nigeria
KIWANJA: Ellis Park, Port Elizabeth
TAREHE: 12 JUNI 2010
SAA: 11 jioni [Bongo]
HABARI ZA TIMU:
Inaaminika Diego Maradona ataibadilisha Fomesheni ya Argentina ili awe na Mastraika Watatu ili kumruhusu Carlos Tevez acheze pamoja na Gonzalo Higuiain wa Real Madrid na Lionel Messi wa FC Barcelona.
Hii ni mechi ya kwanza ya Fainali za Kombe la Dunia kwa Kocha wa Argentina, Diego Maradona, ambae alikuwa Mchezaji Gwiji wa Argentina ambae mara ya mwisho kuichezea Nchi hiyo ilikuwa Mwaka 1994 dhidi ya Nigeria.
Nigeria, walio chini ya Kocha toka Sweden Lars Lagerback, watamkosa Kiungo wa Chelsea John Mikel Obi ambae amejitoa Kikosini baada ya kutopona goti lake na nafasi yake itachukuliwa na Chipukizi Lukman Haruna anaecheza Ufaransa na Klabu ya Monaco.
Argentina wameshaifunga Nigeria mara 3 katika mechi zao za mwisho kati yao ikiwa pamoja na mechi za Makundi kwenye Kombe la Dunia Mwaka 1994 na 2202 ambako walishinda 2-1 na 1-0.
South Korea v Greece
KIWANJA: Nelson Mandela, Port Elizabeth
TAREHE: 12 JUNI 2010
SAA: 8 na nusu mchana [Bongo]
HABARI ZA TIMU:
Mwaka 2002, Korea Kusini walitinga Nusu Fainali za Kombe la Dunia zilipochezwa huko kwao wakishirikiana na Japan lakini Mwaka 2006 walishindwa kuvuka hatua ya Makundi hivyo safari hii watataka kujitutumua kufanya vizuri zaidi.
Mpinzani wa kwanza wa Korea Kusini ni Ugiriki ambao kawaida ni Timu isiyotabirika.
Hii ni mara ya pili kwa Ugiriki kucheza Fainali hizi, mara ya kwanza ilikuwa ni Mwaka 1994 huko Marekani na walifungwa mechi zote 3 za Kundi lao.
Ugiriki walitwaa Ubingwa wa Ulaya Mwaka 2004.
Korea Kusini hawana majeruhi baada ya kupona kwa Nahodha wao Park Ji-sung, Mchezaji wa Manchester United pamoja na mwenziwe Lee Dong-gook.
Ugiriki itamkosa Difenda Vangelis Moras ambae ameumia enka lakini Kiungo Kostantinos Katsouranis anaweza kushika nafasi yake.

No comments:

Powered By Blogger