Monday 20 September 2010

Fabregas nje Wiki 2
Arsenal watafurahi baada ya taarifa kuwa Nahodha wao Cesc Fabregas hakuumia vibaya kama ilivyoogopwa alipotolewa baada ya nusu saa ya mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu walipotoka sare 1-1 na Sunderland.
Fabregas ndie aliewapatia Arsenal bao kwenye mechi hiyo na baada ya hapo akaonekana kuchechemea lakini ripoti za Madaktari zimesema atakuwa nje kwa Wiki mbili akiuguza musuli za paja na hivyo kuna uwezekano mkubwa akacheza BIGI MECHI hapo Oktoba 3 dhidi ya Chelsea huko Stamford Bridge.

No comments:

Powered By Blogger