Sunday 19 September 2010

LIGI KUU ENGLAND: Mechi zijazo
Jumamosi, 25 Septemba 2010
[saa 8 dak 45 mchana]
Man City v Chelsea
[saa 11 jioni]
Arsenal v West Brom
Birmingham v Wigan
Blackpool v Blackburn
Fulham v Everton
Liverpool v Sunderland
West Ham v Tottenham
Jumapili, 26 Septemba 2010
[saa 8 mchana]
Bolton v Man Utd
[saa 10 dak 5 jioni]
Wolverhampton v Aston Villa
[saa 12 dak 10]
Newcastle v Stoke
Fergie: ‘Siku zote sikuwa na wasiwasi na Berbatov!’
SIR ALEX FERGUSON
Sir Alex Ferguson amesisitiza hakuwa na wasiwasi na Dimitar Berbatov na alijua fika Mchezaji huyo ni kipaji na hatari mno na leo ameifikisha patamu baada ya kuwaua wapinzani wao wakubwa Liverpool kwa kufunga bao zote 3 katika ushindi wa 3-2 kwenye mechi ya Ligi Kuu Uwanjani Old Trafford.
Tangu ahamie Manchester United kutoka Tottenham Mwaka 2008 kwa dau kubwa, Berbatov amekuwa akipondwa kwa uchezaji wake lakini Msimu huu ameanza kwa moto mkali kwa kufunga bao 6 katika mechi 5 za Ligi Kuu za Msimu huu.
Ferguson ametamka: “Magazeti yalimshambulia sana Msimu uliopita na hilo hutokea sisi tukinunua Mchezaji kwa bei mbaya na hafungi hetitriki kila mechi! Sikuwa na wasiwasi na yeye, na leo mmeona tena kipaji chake!”
Ferguson akiizungumzia gemu ya leo alisema walipokuwa 2-0 mbele alijiambia mwenyewe hii leo goli 10 na mara ikawa 2-2 lakini mwishowe ulikuwa ushindi mtamu.
Ferguson alitamka: “Hawakucheza lolote Liverpool na walimtegemea Mshika Kibendera awaokoe [akimaanisha goli la kwanza la penalti ambalo Refa Howard Webb alipewa ishara na Mshika Kibendera kutoa penalti]. Van der Sar hakuokoa hata mpira mmoja na Scholes alitawala Kiungo! Tulikuwa moto mbele hasa Berbatov na Nani, hatukustahili kutoshinda mechi hii!”

No comments:

Powered By Blogger