Monday 20 September 2010

Gerrard ajutia kukosa pointi Old Trafford
Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, anahisi walistahili kuondoka Old Trafford hapo jana angalau na pointi moja baada ya kutoka nyuma wakiwa bao 2-0 na kuifanya mechi iwe sare 2-2 lakini Shujaa wa Manchester United Dimitar Berbatov akawaua kwa bao lake la 3.
Gerrard amesema: “Ukiwa Old Trafford na uko nyuma 2-0 kisha ukasawazisha na kuifanya mechi iwe 2-2 ni wazi unapata moyo mpya na unastahili kupata angalau pointi moja!”
Gerrard alisikitika na kipigo cha 3-2 toka kwa Mahasimu wao wakubwa lakini alitamka: “Ni Berbatov ndie aliekuwa tofauti hapo jana. Na goli lake la pili ni la Kimataifa!”
Gerrard ndie alieifungia Liverpool bao zao mbili, moja kwa penati na la pili kwa frikiki.

No comments:

Powered By Blogger