Saturday 25 September 2010

Manchester City 1 Chelsea 0
Jana Roberto Mancini alimsifia Mtaliana mwenzake Carlo Ancelotti na Chelsea yake kuwa watachukua Ubingwa wa Ligi Kuu Msimu huu kirahisi mno lakini leo Mancini na Timu yake tajiri, Manchester City, katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu iliyoanza mapema, waliwatungua Chelsea bao 1-0 kwenye mechi iliyochezwa Uwanja wa City of Manchester.
Ni bao la kipindi cha pili la juhudi binafsi za Carlos Tevez ndilo liliwapa ushindi Man City na kuipa kilio cha kwanza Chelsea ambao walikuwa wameshinda mechi zao zote 5 za Ligi Msimu huu tena nyingine kwa lundo la magoli.

No comments:

Powered By Blogger