Tuesday 29 September 2009

LIGI KUU England: Man City 3 West Ham 1
Ndani ya Uwanja wao City of Manchester, Manchester City jana usiku waliifunga West Ham mabao 3-1 katika mechi pekee ya Ligi Kuu.
Mabao mawili yaliyofungwa na Mchezaji wa zamani wa West Ham ambae baadae alihamia Manchester United, Carlos Tevez, na moja la Petrov ndio yaliyowaua West Ham.
Bao la West Ham lilifungwa na Mshambuliaji wao anaeinukia vizuri kwa sasa Carlton Cole.
Dakika 5 tu tangu mpira uanze krosi ya Petrov ilimkuta Tevez aliefunga huku goli likiwa jeupe na kuwaomba radhi Mashabiki wake wa zamani wa West Ham waliokuwa nyuma ya goli hilo.
Cole akaisawazishia West Ham dakika ya 24 lakini kwenye dakika ya 32 frikiki ya Petrov iliwapa Man City bao la pili.
Carlos Tevez akaihakikishia Timu yake Manchester City ushindi kwa bao la kipindi cha pili dakika ya 61.
Mpaka sasa Man City wako nafasi ya 6 wakiwa wamecheza mechi 5 na wana pointi 12.
FIFA U-20 WORLD CUP Egypt 2009:
MATOKEO MECHI ZA Jumatatu, Septemba 28:
-Nigeria 0 v Spain 2
-French Polynesia- Tahiti 0 v Venezuela 8
-Italy 2 v Trinidad and Tobago 1
-Egypt 1 v Paraguay 2

MECHI ZA LEO Jumanne Septemba 29:
-South Korea v Germany
-USA v Cameroun
-Uruguay v Uzbekistan
-Ghana v England

No comments:

Powered By Blogger