Sunday 27 September 2009

LIGI KUU England: Mvua ya Magoli yazidi kuteremka!!!
Sunderland 5 Wolverhampton 2
Wakiwa nyumbani Stadium of Light, Sunderland leo walishusha kipigo cha mabao 5-2 dhidi ya Wolverhampton na mawili kati ya mabao hayo ya Sunderland yalikuwa ni penalti.
Sunderland walipata bao la kwanza kwa penalti iliyofungwa na Darren Bent na hadi mapumziko bao lilikuwa hilo moja.
Kipindi cha pili tu kuanza, Sunderland wakapata penalti ya pili Mfungaji safari hii akiwa Kenwyne Jones.
Wolves walipata matumaini baada ya mpira kumbabatiza Defenda mpya wa Sunderland kutoka Ghana John Mensah na kutinga wavuni. Dakika chache baadae Wolves wakasawazisha kupitia kwa Straika wao Kevin Doyle.
Lakini Kenwyne Jones akawapeleka mbele tena Sunderland kwa mkwaju mkali na mabao kupitia Michael Turner na Darren Bent yakawamaliza Wolves.
LIGI KUU England itaendelea tena kesho usiku saa 4 saa za bongo wakati Manchester City watakapowakaribisha West Ham Uwanjani City of Manchester.
FIFA U-20 WORLD CUP-EGYPT 2009
Vumbi latimka Jngwani Misri: Mashindano ya Kombe la Dunia la Vijana Chini ya Miaka 20 huko Misri!!
Tangu Alhamisi iliyokwisha, Nchi 24 toka kila kona ya Dunia zipo Nchini Misri kushiriki Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia la Vijana Chini ya Miaka 20 na fungua dimba ilikuwa kati ya Wenyeji Misri na Trinidad and Tobago na wenyeji hao kuibuka kidedea kwa kushinda mabao 4-1.
Nchi hizo zimegawanywa Makundi 6 ya Timu 4 kila moja na Timu mbili kila Kundi zitasonga mbele pamoja na Timu 4 zitakazomaliza kama Washindi wa Tatu kwenye Kundi lakini wenye matokeo bora:
KUNDI A: Egypt, Trinidad & Tobago, Paraguay, Italy.
KUNDI B: Nigeria, Venezuela, Spain, Tahiti
KUNDI C: USA, Germany, Cameroun, South Korea
KUNDI D: Ghana, Uzbekistan, England, Uruguay
KUNDI E: Brazil, Costa Rica, Czech Republic, Australia
KUNDI F: UAE, South Africa, Honduras, Hungary
Ijumaa Septemba 25 kulikuwa na mechi tatu na matokeo ni:
-Paraguay 0 Italy 0
-Nigeria 0 Venezuela 1
-Spain 8 French Polynesia- Tahiti 0
Jana Jumamosi mechi 4:
-USA 0 Germany 3
-Ghana 2 Uzbekistan 1
-Cameroun 2 South Korea 0
-England 0 Uruguay 1
Leo, Jumapili Septemba 27, mechi ni:
-Brazil 5 v Costa Rica 0
-UAE 2 v South Africa 2
-Czech Republic 2 v Australia 1
-Honduras v Hungary
[Matokeo mechi nyingine za leo tutaleta baadae]
Jumatatu, Septemba 28:
-Nigeria v Spain
-French Polynesia- Tahiti v Venezuela
-Italy v Trinidad and Tobago
-Egypt v Paraguay
Jumanne, Septemba 29:
-South Korea v Germany
-USA v Cameroun
-Uruguay v Uzbekistan
-Ghana v England
Jumatano, Septemba 30:
-Australia v Costa Rica
-Brazil v Czech Republic
-Hungary v South Africa
-UAE v Honduras
Alhamisi, Oktoba 1:
-Tahiti v Nigeria
-Venezuela v Spain
-Italy v Egypt
-Trinidad & Tobago v Paraguay
Ijumaa, Oktoba 2:
-Germany v Cameroun
-South Korea v USA
-Uzbekistan v England
-Uruguay v Ghana
Jumamosi, Oktoba 3:
-South Africa v Honduras
-Hungary v UAE
-Australia v Brazil
-Costa Rica v Czech Republic

No comments:

Powered By Blogger