Friday 2 October 2009

FIFA WORLD CUP U20 EGYPT 2009
Wenyeji Egypt, Spain, Paraguay na Venezuela zaingia Raundi ya Pili!!
Wenyeji Egypt wamesonga mbele kuingia Raundi ya Pili ya Kombe la Dunia la Vijana Chini ya Miaka 20 kwa kuwafunga Italy 4-2 na hivyo kuongoza Kundi A.
Paraguay, baada ya kutoka suluhu 0-0 na Trinidad 7 Tobago, imeshika nafasi ya pili na pia kusonga mbele.
Italia ipo nafasi ya 3 na itasubiri kukamilika kwa mechi za Makundi mengine ili kujua kama watafuzu kuingia Raundi ya Pili kwa Tiketi ya Timu zilizoshika nafasi ya 3 bora.
Nigeria waliomaliza nafasi ya 3 Kundi B wapo kwenye hali kama Italia.
Kundi B timu zilizofuzu ni Spain alieshika nafasi ya kwanza na Venezuela wa pili.
MATOKEO:Alhamisi, Oktoba 1:
-Tahiti 0 v Nigeria 5
-Venezuela 0 v Spain 3
-Italy 2 v Egypt 4
-Trinidad & Tobago 0 v Paraguay 0
MECHI ZA LEO Ijumaa, Oktoba 2:
Germany v Cameroun
South Korea v USA
Uruguay v Ghana
Uzbekistan v England

No comments:

Powered By Blogger