Saturday 3 October 2009

LIGI KUU ENGLAND: Baada ya kukosa Mishahara Portsmouth wapata pointi zao za kwanza!!
Wolves 0 Portsmouth 1
Portsmouth ambao wamefungwa mechi zao zote tangu Ligi Kuu ianze msimu huu na juzi kutangazwa Wachezaji hawajalipwa Mishahara na pia Mmiliki wao toka Dubai Sulaiman al Fahim kulazwa hospitalini ili afanyiwe operesheni kutoa vijiwe kwenye figo, leo imepata pointi zake za kwanza tena ikiwa ugenini baada ya kuifunga Wolverhampton bao 1-0.
Goli la ushindi kwa Portsmouth lilifungwa na Hassan Yebda, Mchezaji Mfaransa, ambae yuko Portsmouth kwa mkopo kutoka Benfica.
MATOKEO MECHI ZA LEO Jumamosi, Oktoba 3
Bolton 2 v Tottenham 2
Burnley 2 v Birmingham 1
Hull City 2 v Wigan 1
Wolverhampton 0 v Portsmouth 1

No comments:

Powered By Blogger