Saturday 3 October 2009

MAN U 2 SUNDERLAND 2
Mabingwa Watetezi Manchester United, wakicheza chini ya kiwango, itabidi wamshukuru Anton Ferdinand, mdogo wake Rio Ferdinand aliekuwa benchi la Man U, kwa kujifunga mwenyewe na kuisawazishia Man U dakika za majeruhi.
Mpaka mapumziko Sunderland walikuwa mbele kwa bao 1-0 Mfungaji akiwa Darren Bent dakika ya 8 kwa goli ambalo wengi wanaamini Kipa Ben Foster angeweza kulicheza.
Dimitar Berbatov alisawazisha kipindi cha pili kwa goli zuri sana.
Lakini ni Kipa Ben Foster tena badala ya kupanchi mpira akataka kudaka na kumpa mwanya Straika Kenwyne Jones kuushindilia wavuni.
Kama kawaida, Sir Alex Ferguson alibadilisha Kikosi chake tofauti na kile kilichocheza Jumatano kwenye UEFA CHAMPIONS LEAGUE na hilo liliathiri sana uchezaji.

No comments:

Powered By Blogger