Sunday 27 September 2009

Van Persie aipa ushindi Arsenal lakini Kipa wao 'mpya' Mannone ndie shujaa!!!
Bao la kifundi dakika ya 52 la Robin van Persie liliipa ushindi Arsenal ugenini Craven Cottage walipoifunga timu ngumu Fulham katika mechi ya 'dabi' ya Timu za London ya LIGI KUU lakini ni Kipa wao 'mpya' Chipukizi Vito Mannone toka Italia, anaecheza tu kwa sababu Kipa nambari wani Manuel Almunia na msaidizi wake Lukasz Fabianski hawapo, ndie alieibeba Arsenal kwa kuzuia mabao ya wazi mengi sana.
LEO LIGI KUU [saa 12 jioni saa za bongo]:
Sunderland v Wolverhampton

No comments:

Powered By Blogger