Monday 2 November 2009

Birmingham 0 Manchester City 0
Manchester City inabidi impe pongezi Kipa wao Shay Given kwa kuokoa penalti na kuwafanya watoke suluhu 0-0 na Birmingham Uwanjani Mtakatifu Andrea Mjini Birmingham katika mechi pekee ya Ligi Kuu England iliyochezwa jana.
Hii ni mechi ya 4 mfululizo kwa Man City kutoka suluhu kwenye Ligi Kuu.
Birmingham walitawala mechi hii lakini walishindwa kutumia nafasi zao na mwisho walimaliza wakiwa Wachezaji 10 baada ya Barry Ferguson kupewa Kadi mbili za Njano na hivyo kuonyeshwa Nyekundu.

No comments:

Powered By Blogger