Monday 2 November 2009

Shabiki alievaa kama Kondoo apigwa kibiriti, wenzake wammwagia Bia kuuzima moto huo!!!
Shabiki mwenye umri wa miaka 24 ambae alivaa mavazi kama Kondoo alichomwa moto na kuunguzwa vibaya mikononi na miguuni ndani ya Treni wakati yeye na wenzake wakitoka kuishangilia Timu yao Aberdeen iliyokuwa ikicheza na Hibs mjini Edinburgh huko Scotland.
Baada ya mtu huyo kulipuliwa moto na huku akikimbia ndani ya Treni hiyo iliyokuwa ikisafiri kati ya Edinburgh na Aberdeen, Mashabiki wenzake walimmwagia Bia ili kujaribu kuuzima moto huo.
Polisi inamshikilia mtu mmoja kwa tukio hilo.

No comments:

Powered By Blogger