Monday 22 March 2010

Chelsea walia lakini wajipa matumaini!!
Meneja wa Chelsea Carlo Ancelotti amesisitiza wao bado wana matumaini ya kuwa Mabingwa licha ya jana kupoteza pointi walipotoka suluhu na Blackburn Rovers bao 1-1 na sasa kushikilia nafasi ya 3 wakiwa na pointi 65 kwa mechi 30, Arsenal wakiwa wa pili kwa pointi 67 kwa mechi 31 na Manchester United wakiongoza wakiwa na pointi 69 kwa mechi 31.
Tangu wiki ya pili ya msimu huu kuanza, hii ni mara ya kwanza kwa Chelsea kuwa nje ya Timu mbili za juu na dalili za kupwaya kwao zipo kwenye takwimu kwani wameshinda mechi mbili tu kati ya 8 za ugenini na vilevile wamepata pointi 5 tu katika mechi zao 5 za mwisho za Ligi.
Wiki iliyokwisha Chelsea walitupwa nje ya UEFA CHAMPIONS LEAGUE baada ya kufungwa na Inter Milan na matumaini yao yaliyobaki kupata Vikombe msimu huu ni kwenye Kombe la FA Ligi Kuu tu.
RATIBA LIGI KUU:[saa za bongo]

Jumanne, Machi 23
West Ham v Wolves [saa 5 usiku]
Jumatano, Machi 24

[saa 4 dak 45]
Aston Villa v Sunderland
Man City v Everton
Portsmouth v Chelsea
[saa 5 usiku]
Blackburn v Birmingham

No comments:

Powered By Blogger