Saturday 27 March 2010

Man United yarudi kileleni!!!
• Bolton 0 Man United 4
Wakiwa ugenini Reebok Stadium huku wakijua Wapinzani wao Chelsea wameirarua Aston Villa bao 7-1 na kukwea kileleni katika mechi iliyoanza mapema, Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu, Manchester United, wakicheza bila Mfungaji wao mkuu Wayne Rooney aliepumzishwa pamoja na Beki stadi Rio Ferdinand, nao waliirarua Bolton Wanderers kwa bao 4-0 na kurudi tena kileleni.
Baada ya mechi za leo, MSIMAMO LIGI KUU England huko juu ni kama ifuatavywo:
1. Man United mechi 32 pointi 72
2. Chelsea mechi 32 pointi 71
3. Arsenal mechi 32 pointi 68
4. Tottenham mechi 31 pointi 58
Hadi mapumziko Man United walikuwa mbele kwa bao la Jlloyd Samuel aliejifunga mwenyewe dakika ya 38 katika harakati za kuokoa krosi ya Ryan Giggs.
Kazi nzuri za Nani na Giggs zilizalisha bao 3 kipindi cha pili zilizofungwa na Dimitar Berbatov, mabao mawili na Darren Gibson, bao moja.
Vikosi vilivyoanza:
Bolton: Jaaskelainen, Ricketts, Cahill, Knight, Samuel, Muamba, Lee, Cohen, Wilshere, Elmander, Kevin Davies.
Akiba: Al Habsi, Taylor, Riga, Mark Davies, Klasnic, Andrew O'Brien, Weiss.
Man Utd: Van der Sar, Neville, Vidic, Jonathan Evans, Evra, Fletcher, Scholes, Valencia, Giggs, Nani, Berbatov.
Akiba: Kuszczak, Park, Carrick, Rafael Da Silva, Macheda, Gibson, De Laet.
Refa: Martin Atkinson

No comments:

Powered By Blogger