Tuesday 7 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Kuyt nje wiki kadhaa
Liverpool itamkosa Mshambuliaji wake mpiganaji uwanjani Dirk Kuyt alieumia bega akiwa mazoezini na Timu ya Taifa ya Uholanzi na taarifa za awali zimesema atakuwa nje ya uwanja kwa Wiki kadhaa.
Kuyt, Miaka 30, akiwa kambini na Uholanzi ambao leo wanacheza na Finland kwenye EURO 2012, alianguka vibaya na kufikia bega wakati akijaribu kuunganisha krosi.
Kuumia kwa Kuyt ni pigo kubwa kwa Liverpool ambayo itamkosa katika mechi zijazo dhidi ya Birmingham kwenye Ligi Kuu, Steau Bucharest kwenye EUROPA LIGI na ile BIGI MECHI ya Ligi Kuu dhidi ya Manchester United September 19 huko Old Trafford.

No comments:

Powered By Blogger