Sunday 5 September 2010

PITIA: www.sokainbongo.com

Magazeti England yamvaa Rooney na skandali!!!
Magazeti mawili ya huko England yametoa ripoti kuwa ndoa ya Wayne Rooney ipo majaribuni baada ya kugundulika alitembea na changudoa wakati Mkewe alipokuwa mja mzito.
Imedaiwa Rooney alimjulisha Mkewe jana kuhusu kuvuja kwa Skandali hiyo.
Imedaiwa kuwa Rooney alitembea na Jennifer Thompson, Miaka 21, ambae hutoza Pauni 1,200 kwa usiku mmoja, mara 7 katika kipindi cha Miezi minne.
Licha ya habari hizo kuandikwa kwenye Magazeti, FA imethibitisha Rooney atakuwemo kwenye msafara wa England unaokwenda Uswisi kucheza Mechi ya Makundi ya EURO 2012 dhidi ya Uswisi hapo Jumanne.
Man United yatoa Kikosi cha UEFA CHAMPIONS LIGI
Kikosi cha Wachezaji 30 watakaoiwakilisha Manchester United kwenye Mechi za Makundi ya UEFA CHAMPIONS LIGI kimetangazwa na hawamo Owen Hargreaves na Bebe.
Mchezaji mwingine alieachwa ni Beki Ritchie De Laet.
Wachezaji wapya, Javier Hernandez na Chris Smalling, wamo pamoja na Chipukizi 6 ambao huingizwa kwenye Listi kama Listi B ambao ni Kipa Ben Amos, Mapacha Rafael na Fabio, Oliver Gill, Corry Evans na Federico Macheda.
Kikosi kamili ni:
Van der Sar, Kuszczak, Amos*; Neville, Evra, J.Evans, Ferdinand, W.Brown, Smalling, Vidic, O'Shea, Fabio*, Rafael*, Gill*; Nani, Anderson, Giggs, Park, Carrick, Scholes, Fletcher, Valencia, Gibson, C.Evans*; Berbatov, Rooney, Hernandez, Owen, Obertan, Macheda*.


*Inamaanisha kutoka Listi B ya Chipukizi.

No comments:

Powered By Blogger