Thursday 9 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

LIGI KUU England kurudi dimbani Wikiendi hii!!
Baada ya kuzipisha Mechi za Kimataifa za Nchi za Ulaya kugombea kufuzu Fainali za EURO 2012, patashika za Ligi Kuu zinarudi tena Wikiendi hii kwa Mechi ya kwanza hapo Jumamosi Septemba 11 huko Goodison Park kati ya Wenyeji Everton na Manchester United, mechi ambayo itaanza Saa 8 dakika 45 mchana, bongo taimu.
Mechi hiyo itafuatiwa na mechi 7 ambazo zitaanza Saa 11 jioni zikiwemo za Mabingwa Chelsea wakiwa ugenini kwa West Ham na Arsenal wakiwa nyumbani Emirates kucheza na Bolton Wanderers.
Jumapili kutakuwa na mechi moja tu kati ya Birmingham na Liverpool.
Jumatatu usiku ni mechi kati ya Stoke City na Aston Villa.
RATIBA kamili:
[Saa za Bongo]
Jumamosi, 11 Septemba 2010
[Saa 8 dak 45 mchana]
Everton v Man United
[Saa 11 jioni]
Arsenal v Bolton
Fulham v Wolverhampton
Man City v Blackburn
Newcastle v Blackpool
West Brom v Tottenham
West Ham v Chelsea
Wigan v Sunderland
Jumapili, 12 Septemba 2010
[Saa 12 jioni]
Birmingham v Liverpool
Jumatatu, 13 Septemba 2010
[Saa 4 usiku]
Stoke v Aston Villa

No comments:

Powered By Blogger