Wednesday 8 September 2010

CHEKI: www.sokainbongo.com

Capello afurahishwa na Rooney
Fabio Capello alikuwa na furaha kubwa hapo jana baada ya ushindi wa England wa ugenini wa mabao 3-1 dhidi ya Uswisi kwenye mechi ya Makundi ya EURO 2012 lakini furahi hiyo ilizidi kifani jinsi Wayne Rooney alivyokabiliana na presha ya skandali yake kwa kufunga bao la kwanza.
Capello alitamka baada ya mechi: “Alicheza vizuri. Daima alikuwa ndio kiungo wa mashambulizi yote. Alikuwa na presha kubwa lakini alimudu vyema!”
Ufaransa yazinduka, yashinda ugenini!
Ufaransa, jana ikiwa ugenini, ilizinduka toka lindi la kufungwa na balaa ya migogoro, na kuichapa Bosnia & Herzegovina mabao 2-0 katika mechi ya Makundi ya EURO 2012.
Mabao ya Karim Benzema, dakika ya 72, na Frank Malouda, dakika ya 77, yaliwafufua Vigogo hao wa Ulaya.
EURO 2012
MATOKEO:
Jumanne, 7 Septemba 2010
Turkey 3 Belgium 2
Austria 2 Kazakhstan 0
Germany 6 Azerbaijan 1
Russia 0 Slovakia 1
FYR Macedonia 2 Armenia 2
Republic of Ireland 3 Andorra 1
Serbia 1 Slovenia 1
Italy 5 Faroe Islands 0
Belarus 0 Romania 0
Albania 1 Luxembourg 0
Bosnia & Herzegovina 0 France 2
Sweden 6 San Marino 0
Netherlands 2 Finland 1
Hungary 2 Moldova 1
Georgia 0 Israel 0
Malta 0 Latvia 2
Croatia 0 Greece 0
Bulgaria 0 Montenegro 1
Switzerland 1 England 3
Denmark 1 Iceland 0
Norway 1 Portugal 0
Czech Republic 0 Lithuania 1
Scotland 2 Liechtenstein 1
Mabingwa wa Dunia Spain wapondwa na Argentina
Katika mechi ya kirafiki, Mabingwa wa Dunia, Spain, walichapwa mabao 4-1 na Wenyeji wao Argentina huko Buenos Aires.
Mabao ya Argentina yalifungwa na Lionel Messi na Gonzalo Higuan mapema kisha Kipa wa Liverpool, Pepe Reina, akaipa ‘zawadi’ Argentina pale alipoanguka na kuuruhusu mpira umpite tobo na ndipo Carlos Tevez alipouwahi na kufunga bao la 3.
Baada ya hapo, Spain wakapata bao lao Mfungaji akiwa Fernando Llorente lakini Sergio Aguero akaifungia Argentina bao la 4 dakika za majeruhi.

No comments:

Powered By Blogger