Saturday 28 June 2008

ADEBAYOR: ''nikihama klabu itanufaika!''

Mshambuliaji wa Arsenal Emmanuel Adebayor amekiri hajui atakuwa klabu ipi msimu ujao ingawa anasema ikiwa Arsenal italipwa Pauni milioni 50 wakati wamlinunua yeye kwa Pauni milioni 10 tu bila shaka klabu inapata faida.
Nyota huyo aliefunga goli zaidi ya 30 msimu uliopita alinunuliwa toka Klabu ya Monaco kwa dau la Pauni milioni 7 na siku za karibuni ameonekana kuwa na kauli kigeugeu hasa baada ya Inter Milan kutamka mchezaji huyo ndie yupo nambari wani kwenye listi ya wachezaji wanaotaka kuwasajili.

*********************************************************************************

MSHAMBULIAJI ELMANDER WA SWEDEN ATUA BOLTON
Johan Elamander, miaka 27, alieichezea Sweden kwenye EURO 2008, ametua Bolton Wanderers akitokea Toulouse ya Ufaransa.
Meneja wa Bolton Greg Megson amethibitisha taarifa hizo na kuongeza mchezaji wa kimataifa wa Norway Daniel Braaten atahama Bolton kwenda Toulouse.

*********************************************************************************

MAN CITY WAMSAINI MBRAZIL JO.

Klabu ya Manchester City imemsaini Mbrazil Jo kutoka CSKA Moscow ya Urusi kwa Pauni milioni 19.

Mbrazili huyo mwenye umri wa miaka 21 aliichezea Timu ya Taifa ya Brazil Juni, 2006 kwenye mechi ya ufunguzi wa Uwanja wa Wembley dhidi ya Timu ya Taifa ya Uingereza.

Jo amefunga goli 30 katika mechi 53 alizochezea CSKA Moscow na anategemewa kusaini mkataba wa miaka minne.

No comments:

Powered By Blogger