Sunday 22 June 2008


KIKOSI CHA UTURUKI MASHAKANI
Kipa wa akiba huenda akacheza mbele

UEFA wametamka hawawezi kuwaruhusu Uturuki kuita wachezaji wapya kuja kwenye EURO 2008 kufuatia timu yao kukabiliwa na majeruhi wengi na wengine kufungiwa mechi kutokana na kadi.
Hali hii inamaanisha huenda Uturuki wakalazimika kumchezesha Kipa wa akibaTolga Zengin kama mchezaji wa mbele.
UEFA imesisitiza kanuni zinatamka wazi huwezi kuita mchezaji mpya baada ya mechi ya kwanza ya EURO 2008 na wameongeza wangeita kikao cha dharura pale tu timu ingebakiwa na wachezaji wanane tu.
Uturuki wanakutana na Ujerumani Nusu Fainali siku ya Jumatano.
Meneja Fatih Terim amesema wachezaji sita muhimu ni majeruhi wakiwa pamoja na mshambuliaji nyota Nihat Kahveci wakati Kipa nambari wani Volkan Demirel, Tuncay Sanli, Arda Turan na Emre Asik wamefungiwa.

No comments:

Powered By Blogger