Sunday 22 June 2008

Scolari – Ronaldo ana ndoto na Real
Bosi mpya wa Chelsea anategemea nyota wa Man United kuhama
Luiz Felipe Scolari amesisitiza Manchester United hawawezi kumzuia Cristiano Ronaldo asihamie Real Madrid.
Kocha huyo anaeiacha Timu ya Taifa ya Ureno Julai 1 na kuhamia Chelsea wapinzani wa Man United kwenye LIGI KUU anadai anamfahamu vizuri Ronaldo na ndio maana amesisitiza Ronaldo atahama.
Kauli hii ya Mbrazil huyo inadhirisha zaidi kile wanachoamini Man United kuwa Scolari ni mchochezi mkubwa anaemshawishi Ronaldo kuhama ili kuibomoa Man United ili yeye apate upinzani hafifu akiwa kwenye timu yake mpya ya Chelsea.
Mpaka sasa Man United wamesisitiza Ronaldo hauzwi na hawaingia kwenye majadiliano na yeyote kuhusu kuuzwa nyota huyo
.

No comments:

Powered By Blogger