Thursday 26 June 2008




Germany 3-2 Turkey
GOLI DAKIKA YA MWISHO LAWAUA WATURUKI!
RADI ZAKATISHA MATANGAZO!
Beki wa kushoto Philipp Lahm alifunga bao la ushindi katika dakika ya mwisho ya mchezo na kuwaingiza Ujerumani FAINALI ya EURO 2008 ambapo watakutana na Uhispania au Urusi wanaocheza leo.
Uturuki iliyoonekana dhahiri ni timu bora ilipata bao la kwanza dakika ya 22 lililofungwa na Uqur Boral lakini Ujerumani ikasawazisha dakika ya 27 kwa goli la Schweinsteiger.
Miroslav Klose akafunga kwa kichwa goli la pili la Ujerumani kwenye dakika ya 79 na Mturuki Senturk akasawazisha dakika ya 86.
Wengi wakiamini dakika za nyongeza 30 zitachezwa, Wajerumani walicheza soka safi lililoishia kwa beki wa kushoto Philipp Lahm kufunga kwenye dakika ya 89.
Hakika Waturuki walikufa kishujaa kwani mbali ya kuwa na majeruhi wengi na wachezaa kadhaa kufungiwa ilikuwa wazi walitawala mchezo. Pengine bahati haikuwa yao kwani ‘Mwingereza’, mchezaji wa zamani wa Sheffield United Colin Kazim-Richards ambae siku hizi hujiita Kazim Kazima baada ya kuamua kuchezea Uturuki kwa kuwa na damu ya Kituruki, alipiga shuti dakika ya 12 lililompita Kipa Jens Lehmann na kugonga mwamba. Na tena dakika ya 22 aligonga mwamba!
Wapenzi wengi katika pembe kadhaa za dunia walikosa matangazo ya TV kwa muda baada ya radi na mvua kukatiza matangazo.
Germany: Lehmann, Friedrich, Mertesacker, Metzelder, Lahm, Hitzlsperger, Rolfes (Frings 46), Schweinsteiger, Ballack, Podolski, Klose (Jansen 90).
Akiba: Enke, Adler, Fritz, Westermann, Gomez, Neuville, Trochowski, Borowski, Odonkor, Kuranyi.
MAGOLI: Schweinsteiger 27, Klose 79, Lahm 90.
Turkey: Rustu, Sarioglu, Topal, Zan, Balta, Aurelio, Kazim-Richards (Metin 90), Altintop, Akman (Erdinc 81), Boral (Karadeniz 84), Senturk.
Akiba: Zengin, Cetin, Emre, Gungor, Nihat.
KADI: Senturk.
MAGOLI:
Boral 22, Senturk 86.
WATAZAMAJI: 40,000
REFA: Massimo Busacca (Switzerland).

No comments:

Powered By Blogger