Tuesday 24 June 2008

Paul Ince atambulishwa rasmi Meneja Blackburn Rovers
Mwenyekiti wa Blackburn Rovers John Williams amemtangaza rasmi Paul Ince kuwa Meneja mpya wa klabu yake kuchukua nafasi ya Mark Hughes aliehamia Manchester City.Ince, mwenye umri wa miaka 40, amepewa mkataba wa miaka mitatu na anaweka rekodi ya kuwa Meneja wa kwanza 'mweusi' katika historia ya LIGI KUU UINGEREZA.
Blackburn Rovers ilipata kibali maalum kutoka FA, ambacho ni Chama cha Soka Uingereza, kumtumia Paul Ince bila ya yeye kuwa na LESENI YA UKOCHA YA UEFA PRO.
Leseni hii inahitajika kwa Mameneja wote wa ligi za juu za nchi nyingi Ulaya.Ili kupata leseni hii inabidi upate masomo maalum ya zaidi ya masaa 240 na kawaida huchukua mwaka mmoja kuhitimu. Mkataba wa Paul Ince na Blackburn Rovers una kipengele kwamba lazima Ince ahitimu hiyo LESENI YA UKOCHA YA UEFA PRO

No comments:

Powered By Blogger