Sunday 22 June 2008


Netherlands 1-3 Russia
Urusi, wakiongozwa na Meneja Mholanzi Guus Hiddink, jana waliwaendesha mchakamchaka Uholanzi timu iliyodhaniwa bora kwenye EURO 2008 na kuwabwaga kwa mabao 3-1 kwenye kandanda iliyochezwa dakika 120.
Roman Pavlyuchenko aliwawafungia Urusi bao la kwanza lakini Ruud van Nistelrooy alisawazisha na mpira ukingia dakika za nyongeza.
Dimitri Torbinski na Andrei Arshavin wakahakikisha ushindi kwa Urusi kwa kupachika bao la pili na la tatu.
Bosi wa Urusi Guus Hiddink aliisifia timu yake: "Sitaki kutumia maneno makubwa. Lakini ni maajabu. Nasikia fahari kwa vijana wangu. Kwa nguvu, utaalam na mbinu tuliwazidi Waholanzi wenzangu!'
MECHI YA LEO:
ROBO FAINALI: Spain v Italy
Kocha wa Uhispania Luis Aragones atakirudisha kikosi chake cha kwanza kwenye mechi hii ya Robo Fainali dhidi ya Italia alichokipumzisha kwenye mechi ya kukamilisha ratiba ambayo waliwafunga Ugiriki 2-1.
Italia wana tatizo kubwa la kuwakosa viungo Gennaro Gattuso na Andrea Pirlo ambao wote wana kadi na hawaruhusiwi kucheza mechi hii. Badala yake Alberto Aquilan na Massimo Ambrosini wanategemewa kuanza huku Daniele De Rossi na Simone Perrotta pia wana nafasi kubwa ya kucheza.

NUSU FAINALI
JUMATANO
25 JUNI
UJERUMANI V UTURUKI
ALHAMISI
26 JUNI
URUSI V SPAIN/ITALIA

No comments:

Powered By Blogger