Tuesday 24 June 2008

Real wang’aka hawawezi kuvunja benki kwa Ronaldo!
Nae Carlos Queiroz adai: "Manchester United ni spesho, Ronaldo atabaki!!"
Ramon Calderon, Rais wa Real Madrid, amegeuka na kudai hawawezi kuvunja benki ili kumnunua Ronaldo.
Imekuwa ikivumishwa kwamba Real wako tayari kuvunja rekodi ya dunia ya kumnunua mchezaji na kuwalipa Manchester United Pauni za Kiingereza milioni 80 ili kumnunua Cristiano Ronaldo.

Real kwa sasa ndio wanaoshikilia rekodi hiyo ya kumnunua mchezaji kwa bei ghali sana pale walipomnunua Zinedine Zidane mwaka 2001 kwa Pauni za Kiingereza milioni 46.
Hata hivyo Ramon Calderon amekataa na kudai hamna ‘ishu’ ya Ronaldo kwa sababu kwanza Manchester United hawataki kumuuza na pili wao hawawezi kumnunua mchezaji yeyote yule kwa dau hilo.
Wakati huohuo, Wareno wawili wenzake Ronaldo ambao wako pamoja nae Manchester United wameibuka na kumsihi abaki Manchester.
Mchezaji Nani amekaririwa akisema: ‘Ni dhahiri nataka abaki. Alinisaidia sana nilipowasili Man U.’
Nae Meneja msaidizi wa Man U Carlos Queiroz ana matumaini kuwa mapenzi ya Klabu ya Manchester United kwa Ronaldo yatamfanya abakie Old Trafford klabu aliyojiunga mwaka 2003 akitokea Sporting Lisbon ya Ureno.
"Manchester United ni spesho," Queiroz aliiambia Redio ya Kireno iitwayo Renascenca. "Kwa sababu hiyo tunajua namna ya kumzunguka na kumfariji Cristiano kwa upendo na kila hali inayobidi na hali hii hawezi kuipata kwingine kokote.’

No comments:

Powered By Blogger