Tuesday 24 June 2008

WATURUKI WANA MOYO WA KIJERUMANI: Ballack akiri!
Nahodha wa Ujeruman Michael Ballack anaamini wapinzani wao kwenye NUSU FAINALI ya EURO 2008 itakayochezwa kesho Uturuki wana moyo wa kijasiri wa Kijerumani na hivyo mechi hiyo itakuwa ngumu sana kwao.
Ingawa Ujerumani wanapewa nafasi kubwa ya kushinda, Ballack ambae ni mchezaji wa Klabu ya Chelsea anakiri: "Wana moyo, imani na umadhubuti wa Kijerumani! Hawakati tamaa na ndio maana wamefunga magoli mengi mwishoni mwa mechi –kitu ambacho ni Ujerumani pekee hukifanya katika mashindano makubwa."
Hata hivyo kikosi cha Uturusi kina hali ngumu sana na huenda wakalazimika kumchezesha Kipa wa akiba Tolga Zengin kama mchezaji wa mbele kutokana na wachezaji sita muhimu kuwa majeruhi wakiwa pamoja na mshambuliaji nyota Nihat Kahveci wakati Kipa nambari wani Volkan Demirel, Tuncay Sanli, Arda Turan na Emre Asik wamefungiwa.

***********************************************************************************
Ronaldo aenda likizo na kuacha fumbo!
Mapaparazi, hasa wa Kihispania wanaoshabikia Ronaldo kuhamia Real Madrid, wamepigwa bumbuwazi baada ya nyota huyo kuingia mitini na kwenda likizo ya wiki tatu kuanzia jana bila ya ufafanuzi kuhusu hatma yake.
Wengi walitegemea jana kutakuwa na habari za kuvunja shoka lakini walipigwa butaa waliposikia Ronaldo sasa anaenda mapumzikoni.
Wakati Ronaldo anaanza likizo ya wiki tatu mapaparazi sasa watawaandama Meneja wa Man U Sir Alex Ferguson na Mkurugenzi Mkuu wa klabu David Gill mara tu watakaporudi toka likizo zao wiki ijayo ili kudadisi mambo.

No comments:

Powered By Blogger