Thursday 26 June 2008

LIPPI ATEULIWA TENA KUWA MENEJA WA ITALY
Marcello Lippi alieiongoza Italia kuchukua Kombe la Dunia mwaka 2006 huko Berlin, Ujerumani amechaguliwa tena kuwa Meneja wa Italy kuchukua nafasi ya Roberto Donadoni alieachia ngazi kufuatia Italy kutolewa kwenye Robo Fainali ya EURO 2008 na Spain kwa penalti 4-2 baada ya dakika 120 za mchezo kuwa suluhu 0-0.
Lippi, umri miaka 60, hajafanya kazi yeyote tangu alipojiondoa madarakani mara baada ya Italy kunyakua Kombe la Dunia huo mwaka 2006.

No comments:

Powered By Blogger