Thursday 26 June 2008




LIGI KUU UINGEREZA YAMTEUA REFA 'MTOTO'!
Bosi wa Marefa nchini Uingereza Keith Hackett ametangaza kumchagua Stuart Attwell, mwenye umri wa miaka 25, kuwa miongoni mwa Marefa watakaochezesha LIGI KUU UINGEREZA msimu wa 2008/9 unaoanza tarehe 16 Agosti 2008.
Keith Hackett amethibitisha Refa huyo ndie atakuwa Refa mdogo kupita wote kuchezesha LIGI KUU. Refa huyu aliaanza kazi ya urefa mwaka 1998 na mwaka 2007 alipata promosheni na kuingizwa kwenye Listi ya Marefa wa Taifa huko Uingereza.

No comments:

Powered By Blogger