Monday 23 June 2008


Spain 0-0 Italy

Italia wang'oka kawa penalti 4-2

Spain kukutana tena na Urusi!

Spain wamewatoa Italy 4-2 kwa penalti na kuingia NUSU FAINALI ya EURO 2008 kucheza na Urusi ikiwa ni mara ya pili kwa Spain na Urusi kukutana katika mashindano haya.
Mechi ya kwanza ilikuwa kwenye KUNDI D wakati Urusi ilipobamizwa 4-1 ingawa Warusi wanaweza kujipa moyo kwamba katika mechi hiyo staa wao mkubwa Andrei Arshavin hakucheza kwani alikuwa kafungiwa.
Mechi kati ya Spain na Italy ilikuwa ngumu na nafasi zilikuwa chache na hata dakika 120 hazikutoa mshindi.
Katika penalti Kipa wa Spain Iker Casilla alikuwa shujaa kwa kuokoa penalti za Daniele de Rossi na Antonio di Natale.
Ushindi huu wa Spain utakuwa mtamu sana kwa Wahispania hasa wakikumbuka katika mashindano makubwa matatu yaliyopita, yaani Kombe la Dunia mwaka 1986 na 2002 na Euro 1996, walitolewa Robo Fainali - na mara zote kwa penalti na tarehe ikiwa hiyohiyo moja, yaani tarehe 22 Juni kama ya jana!

NUSU FAINALI
JUMATANO
25 JUNI
UJERUMANI V UTURUKI
ALHAMISI
26 JUNI
URUSI V SPAIN
FAINALI
JUMAPILI
29 JUNI
MSHINDI WA UJERUMANI V UTURUKI V URUSI V SPAIN


No comments:

Powered By Blogger