Monday 23 June 2008


Pele aporwa na vibaka!
Pele, Mbrazil veterani na nyota maarufu sana duniani, alitishiwa bastola na vibaka na kuporwa mkufu wa dhahabu, simu na saa karibu na mji wa Santos, Brazil tarehe 13 Juni 2008.
Pele, jina kamili Edison Arantes do Nascimento, mwenye miaka 67 alikuwa abiria kwenye gari dogo akielekea nyumbani kwake na gari hiyo ikalazimishwa kusimama na genge la vibaka wasiopungua 10 waliokuwa wamebeba bastola na visu.
Vibaka hao baada ya kumpora ndio wakagundua kumbe ni Pele wakaamua kumrudishia baadhi ya vitu.
Pele, ambae aliisaidia sana Brazil kunyakua Vikombe vitatu vya Dunia kati ya vitano ambavyo inavyo, hakuripoti tukio hilo Polisi.
Taifa la Brazil linamtambua kisheria Pele kama ni ‘HAZINA YA TAIFA’ na Kamati ya Olympiki ya Dunia mwaka 1999 ilimpigia kura kwamba ndie MWANAMICHEZO BORA WA KARNE!

No comments:

Powered By Blogger