Tuesday 24 June 2008

Liverpool waanza kujenga uwanja mpya
Klabu ya Liverpool imeanza ujenzi wa uwanja mpya kwa gharama ya Pauni £350 milioni jirani na Uwanja wa sasa wa Anfield.
Klabu hiyo imeruhusiwa kuanza ujenzi huku mkataba wa hati miliki ya ardhi wa miaka 999 ukiendelea kujadiliwa na serikali.
Kibali hicho kinaruhusu ujenzi wa uwanja utakaoingiza watazamaji 60,000 na kinaweza kupanuliwa kufikia watu 73,000 baadae. Ufunguzi wa uwanja huo mpya unategemewa kuwa Agosti, 2011.
Hadi sasa klabu inayoongoza kwa kuwa na uwanja mkubwa unaoingiza watu wengi ni Manchester United na uwanja wao Old Trafford ukipakia watu 76,000, Arsenal na Emirates watu 60,000, Newcastle na wa kwao St James Park watu 52,000, Manchester City na The City of Manchester Stadium watu 47,000, Liverpool na Anfield watu 45,000 huku Chelsea na Stamford Bridge yao watu 42,000.

No comments:

Powered By Blogger