Tuesday 24 June 2008

JUMATANO, JUNI 25: NUSU FAINALI YA 1: Germany v Turkey
UWANJA: St Jakob-Park, Basel, SWITZERLAND

Kocha wa Ujerumani Joachim Low amesema kiungo Torsten Frings anaweza kucheza mbali ya kuvunjika mbavu katika mechi za makundi na kuikosa mechi ya ROBO FAINALI ambayo waliifunga Ureno. Ukiacha hilo, Ujerumani wana kikosi chao kamili bila ya majeruhi au athari nyingine.
Uturuki wanakabiliwa na majeruhi wengi pamoja na wachezaji kadhaa kufungiwa kwa kuwa na kadi na hivyo wanaweza wakawa na kikosi chenye wachezaji 13 tu wa mbele kuwakabili Ujerumani.
Juhudi zao za kujaribu kukata rufaa ili Kipa nambari wani na Nahodha wao Volkan Demirel afunguliwe baada ya kufungiwa mechi mbili baada ya kadi nyekundu kwenye mechi na Czech Republic zimekataliwa na UEFA.
Meneja wa Uturuki Fatih Terim amesema inawezekana akamchezesha kipa wa tatu wa akiba Tolgan Zengin kwenye mechi hii: "Anaweza kuingia mwisho kabisa wa mechi kwenye ulinzi kama beki wa nyuma kabisa au mshambuliaji wa mbele kabisa."
Uso kwa uso
Ujerumani na Uturuki washakutana mara 17 huku Ujerumani akishinda mechi 11 na kupoteza 3 tu.
Waturuki hawajafungwa na Ujerumani katika mechi tatu zao za mwisho kukutana ambazo walishinda mbili na kutoka droo moja.
Ushindi wa mwisho wa Ujerumani dhidi ya Waturuki ulikuja Mei 1992 waliposhinda 1-0 kwenye mechi ya kirafiki.
Mara ya mwisho kukutana kwenye mashindano makubwa ilikuwa kwenye Kombe la Dunia mwaka 1954 nchini Uswisi na wakati huo ikiwa inaitwa Ujerumani Magharibi [wakati huo kulikuwa na Ujerumani mbili-moja Magharibi na nyingine Mashariki] na Ujerumani ilishinda 4-1 and 7-2 katika mechi mbili za mashindano hayo.
Mechi ya mwisho kabisa kukutana ni katika mechi ya kirafiki Oktoba 2005 mjini Instanbul, Uturuki na Uturuki walishinda 2-1.
Waamuzi
Refa: Massimo Busacca, Wasaidizi: Matthias Arnet, Stephane Cuhat (Wote kutoka Uswisi),
Refa wa akiba: Peter Frojdfeldt (Sweden)

No comments:

Powered By Blogger